
Chid Benz akiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar.
Chid Benzi akitoka lango la mahakama ya Kisutu.
..Akifungua mlango wa gari lililokuwa likimsubiri.
HATIMAYE msanii wa
muziki wa kizazi kipya, Rashid Makwiro 'Chid Benz' leo asubuhi amepata
dhamana baada ya kutimiza masharti ya kesi yake ya kukamatwa na dawa za
kulevya.
Msanii
huyo, jana alipandishwa kizimbani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
jijini Dar es Salaam na kusomewa mashitaka matatu ya kukutwa na madawa
ya kulevya ambapo alishindwa kutimiza masharti ya dhamana ya shilingi
milioni 1 pamoja na wadhamini wawili wasiokuwana hatia.
Kesi yake itasikilizwa tena Novemba 11 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment