
Roketi Antares ikilipuka.

Taswira baada ya mlipuko huo.

Roketi hiyo wakati ikjiandaa kupaa.
ROKETI ya safari za anga za juu iliyokuwa ikielekea Kituo cha
Kimataifa cha Anga za Juu imelipuka wakati ikiruka kutoka Jimbo la
Virginia nchini Marekani.
Roketi hiyo iitwayo Antares, yenye urefu wa ghorofa 14 ikiwa
iliyotengenezwa na Shirika la Orbital Sciences Corp, ililipuka sekunde
chache baada ya kuruka katika kituo cha Wallops Flight Facility.
Chanzo cha kulipuka kwa roketi hiyo ya mizigo bado hakijafahamika.
Antares ilitarajiwa kuwa roketi ya tatu kupewa kandarasi na shirika
la taifa la kusimamia safari za anga za juu la Marekani, NASA.
Roketi hiyo ilitarajiwa kubeba takribani kilo 2,200 za shehena kwa
ajili ya wanaanga sita walioko katika Kituo cha Kimataifa cha Anga za
Juu.
"Tutajua kilichotokea hivi karibuni na tutaendelea vizuri na mipango
yetu," amesema Frank Culbertson, Makamu wa Rais Mtendaji wa Shirika la
Orbital Sciences.
"Wote tumeona hili jambo likitokea kabla katika shughuli zetu na
tumeona kampuni husika zikiimarika kutokana na tukio kama hili, na
tutafanya vivyo hivyo" aliongeza Frank.
No comments:
Post a Comment