Wednesday, 29 October 2014

LORI LA MAFUTA LAANGUKA DAR LATEKETEA KWA MOTO


 
Mashuhuda wakieleza yaliyotokea.
 
Wafanyakazi kampuni inayomiliki lori hilo ambayo bado haijafahamika, wakifanya tathmini ya hasara iliyopatikana.
 
Sehemu ya matairi ilivyobaki.
 
Sehemu ya juu ilivyoungua.
 
Maofisa wa polisi wakijadiliana la  kufanya.
Wakielekea eneo la tukio baada ya kufikia muafaka 
Afisa wa polisi akimpa maelekezo askari wa usalama barabarani.
 
Mashuhuda kila mmoja akieleza lake.
 
Madereva wa bodaboda wakiwa wameacha shughuli zao ili kushuhudia tukio hilo.
LORI la mafuta aina ya Scania likiwa limesheheni dizeli likitokea bandarini jijini Dar es Salaam kuelekea mikoani, liligonga tuta katika Barabara ya Morogoro, eneo la Kimara-Baruti,  likapoteza mwelekeo na kupinduka kisha kuwaka moto na kuteketea kabisa.
Wakati lori hilo likiwaka, mafuta yenye moto yalisambaa na kutaka kuunguza nyumba za jirani lakini Kikosi cha Uokoaji na Zima Moto cha Halmashauri ya Jiji, kiliwahi kufika eneo la tukio na kuudhibiti moto huo.
Tukio hilo limesababisha usumbufu mkubwa kwa magari yanayotumia njia hiyo kutokana na sehemu hiyo kupitika kwa shida.

No comments:

Post a Comment