Friday, 7 November 2014

MAPANGA YAANZA MBEYA CITY.

Mashabiki wa...
Mbeya City.
WAKATI ikiendelea kuwa na matokeo mabaya katika Ligi Kuu Bara, uongozi wa Mbeya City umemkabidhi madaraka kocha wao, Juma Mwambusi kuwaondoa kikosini wachezaji watakaoonekana hawana umuhimu klabuni hapo wakati wa dirisha dogo la usajili.
Emmanuel Kimbe ambaye ni katibu wa Mbeya City, ameliambia amefunguka na kusema kuwa, kinachotakiwa ni mwalimu kuwasilisha ripoti kisha kama kuna wachezaji wa kuondolewa au kuongezwa, wao wataifanyia kazi.
“Tunasubiri mapumziko ya usajili wa dirisha dogo ili kupata ripoti ya kocha na hapo ndipo tutakapojua nani aondoke na nani aongezwe katika usajili, lengo letu ni kuona timu inakuwa bora,” alisema Kimbe.Mbeya City imefungwa michezo mitatu katika ligi kuu na sare mbili, huku ikiwa imeshinda mchezo mmoja.

No comments:

Post a Comment