Friday, 7 November 2014

AZAM: KIPRE, KAPOMBE WAPO SOKONI.

Mchezaji wa Azam, Kipre Tchetche.
KUELEKEA dirisha dogo la usajili, Azam FC imefunguka kuwa ipo tayari kuwauza wachezaji wake Shomari Kapombe, Kipre Tchetche na Mwadini Ali endapo kutatokea klabu nyingine inayoweza kutoa dau zuri...

Hatua hiyo inakuja hivi karibuni, baada ya kuripotiwa kuwa Kipre anaweza kuondoka klabuni hapo kuelekea nchini Malaysia, Sri Lanka au katika Klabu ya Sofapaka ya nchini Kenya.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Katibu Mkuu wa Azam FC, Idrissa Nassor, alisema kuwa kama kuna timu itawahitaji wachezaji wao watawauza lakini kwa dau la uhakika kutokana na viwango vyao.
Nassor alisema kuwa mpaka sasa hakuna mchezaji wa kikosi hicho ambaye amemaliza mkataba wake ili kuweza kuondoka katika klabu hiyo labda mpaka pale msimu utakapokuwa unamalizika.
Mchezaji wa Azam Shomari Kapombe.
“Kama kuna timu yoyote ya ndani au nje itawahitaji wachezaji wetu kama Kipre Tchetche, Shomari Kapombe au Mwadini Ali hatuna tatizo, kikubwa ni maelewano, ingawa wachezaji hawa wana mkataba,” alisema Nassor.

No comments:

Post a Comment