Monday, 10 November 2014

KIEMBA, CHANONGO NJE SIMBA


Mchezaji wa Simba, Amri Kiemba.
BAADA ya mchakato wa kuchanganua mambo, kuna asilimia kubwa Kamati ya Utendaji ya Simba ikatoa majibu ya kuwaondoa wachezaji wawili, Amri Kiemba na Haruna Chanongo.Lakini kiungo mkongwe, Shabani Kisiga anapewa nafasi ya kuendelea kuitumikia timu hiyo kutokana na utetezi wake..
Watatu hao walisimamishwa kwa tuhuma za utovu wa nidhamu na kucheza chini ya kiwango na baadaye wakaonyesha utovu wa nidhamu kwa kushindwa kutokea kwenye kikao cha viongozi.“Wachezaji walivyojieleza, inaonekana Kisiga amekuwa hana matatizo makubwa na hata imefikia kwamba atasamehewa.
Mchezaji wa Simba, Haruna Chanongo.
“Lakini Kiemba na Chanongo, kuna zaidi ya asilimia tisini wataondoka Simba. Sijui, labda mambo yabadilike tena mwishoni, si unajua uongozi ni kitu cha watu wengi,” kilieleza chanzo.“Watu wengi hawajui uongozi unafanya nini, ukweli ni kwamba uongozi unajua kila kitu, unajua mambo mengi kuliko watu wanavyojua na wala hauna nia ya kumuonea mtu, lengo kuisaidia timu.”
Uongozi wa Simba, bado haujatangaza lolote kuhusiana na hilo lakini utakuwa na nafasi ya kumalizia uamuzi huo na kuutangaza ndani ya wiki hii.
Mara baada ya mchezo wa jana ambao Simba walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi Ruvu Shooting, Kisiga pekee ndiye alishuka chini baada ya mchezo kumalizika na kwenda kuwapongeza wachezaji wenzake vyumbani.Hata hivyo, kocha wa Simba, Patrick Phiri, alipoulizwa kama suala lake limekwisha, alisema waulizwe viongozi.

No comments:

Post a Comment