Wednesday, 31 December 2014

PHIRI AONDOKA SIMBA KWA MAJONZI


Kocha Patrick Phiri.
KOCHA Patrick Phiri amesema amesikitishwa na taarifa za...
kuachishwa kazi Simba, lakini angependa kumalizana vizuri na uongozi wa klabu hiyo.Phiri raia wa Zambia amesema tayari amepewa taarifa hizo na mmoja wa viongozi wa Simba, lakini si taarifa rasmi ya barua.
“Nimeelezwa, si kitu cha furaha. Nasikia majonzi kwa kuwa niliona ninaweza kubadilisha mambo baada ya kupata kikosi kipya.“Nilikuta kikosi kipya, tukawa tunaanza kuzoeana lakini tukafanya tena mabadiliko, hivyo ndiyo tulikuwa tumeanza kutengeneza timu tena, tukafungwa na Kagera.
“Sidhani kama tumefanya vibaya sana, lakini siwezi kuzuia uongozi unataka nini. Vizuri tumalizane vizuri,” alisema.Hata hivyo, Phiri alisisitiza ataendelea kusubiri apate taarifa ya maandishi na stahiki zake.
“Kwa mtu aliyeniambia, najua haiwezi kuwa mzaha. Hivyo nitasubiri barua ili kudhibitisha, pia nitapokea madai yangu, basi nitaaga vizuri na kurejea nyumbani.”Nafasi ya Phiri inachukuliwa na Goran Kuponovic raia wa Serbia anayetua leo asubuhi akitokea Hungary.

No comments:

Post a Comment