Tuesday, 11 November 2014

RAIS MICHAEL SATA KUZIKWA LEO

Rais Michael Sata enzi za uhai wake.
Mazishi ya kitaifa yanafanyika nchini Zambia kumuaga hayati Rais wa nchi hiyo Michael Sata aliyefariki hospitalini mjini London Uingereza mwezi jana.Sata alikuwa na umri wa miaka 77...

Katika wiki chache zilizopita, wanachi wamekuwa wakitoa heshima zao za mwisho kwa kiongozi huyo ambaye mwili wake ulikuwa umelazwa katika majengo ya bunge.
Mwili wa Rais Michael Satta ukipewa heshima za mwisho.
Rais Sata alifariki akipokea matibabu mjini London UingerezaMazishi yanayofanyika mjini Lusaka yatahudhuriwa na viongozi mbali mbali wa kikanda.Rais Sata atazikwa katika eneo lenye makaburi yaliyotengewa Marais wa nchi hiyo.Taifa hilo kwa sasa linaongozwa na kaimu Rais huku uchaguzi mkuu ukipangwa kufanyika katika muda wa miezi michache ijayo.

No comments:

Post a Comment