Friday, 14 November 2014

NGASSA ABAKI NCHINI ILI AFUNGE NDOA!

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho...
Ngassa na mkewe wakiwa wenye nyuso zenye furaha baada ya kufunga ndoa.
BAADA ya kuelezwa kuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa ameshindwa kusafiri na Taifa Stars kwenda nchini Afrika Kusini kutokana na matatizo ya kifamilia, imebainika kuwa mchezaji huyo amebaki nchini ili afunge ndoa.
Stars ipo Afrika Kusini kwa ajili ya kambi ya muda kisha ikitarajiwa kuelekea nchini Swaziland, leo kwa ajili ya mechi ya kirafiki baina ya mataifa hayo itakayopigwa kwenye Uwanja wa Somhlolo jijini Mbabane.
Rafiki wa karibu wa Ngassa alizungumza na mwandishi na kusema kuwa, Ngassa hana matatizo ya kifamilia ila aliomba kubaki nchini kwa kuwa alikuwa katika hatua za mwisho za kufunga ndoa.
“Ngassa amebaki ili afunge ndoa, shughuli yote itafanyika kesho (leo Ijumaa) hapahapa Dar, nafikiri hii itakuwa ndoa yake ya tatu,” alisema rafiki huyo.
Ngassa alipotafutwa kwa njia ya simu ili aweze kuzungumzia ishu iyo lakini simu zake zote zilikuwa hazipatikani, ndipo akatafutwa baba yake mzazi, Khalfan Ngassa  ambaye alikuwa na haya ya kusema:
“Ndiyo anataka kufunga ndoa, hii itakuwa ndoa yake ya pili siyo ya tatu, ile ya kwanza ndiyo ya yule mwanamke waliyevurugana na kesi yao ipo mahakamani, huyo mnayesema wa pili hakufunga naye ndoa bali ni mzazi mwenziye, huyu wa sasa ndiye atakuwa mke halali.”

No comments:

Post a Comment