
Msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka
BAADA ya msanii wa filamu Bongo, Rose Ndauka
kuonekana akijiachia viwanja mbalimbali tofauti na alivyokuwa akiishi
awali, mzazi mwenzake, Malick Bandawe, ameibuka na kumfungukia kuwa
aachwe ajirushe....
Malick alifungua kinywa kufuatia madai kwamba alipokuwa akiishi na Rose alikuwa akimpa sheria kali na kumkataza kwenda ‘out’ ndiyo maana alikuwa hajiachii kama ilivyo sasa na hiyo ni moja ya sababu zilizosababisha uhusiano wao kuvunjika.
“Mimi siyo mkali wala sina sheria hizo ninazoambiwa ila nilikuwa nachukua muda mwingi sana kuzungumza na Rose na ninaamini amejifunza mengi sana mazuri ambayo akiyazingatia yatamsaidia maishani.
“Sababu za Rose kujiachia hivyo ni kutokana na maisha ambayo tulikuwa tunaishi hivyo anahitaji muda atatulia na atakuwa sawa na hapo ndipo atakapoanza kuyafanyia kazi yale mazuri aliyoyapata kutoka kwangu, sitegemei yeye kufanya mabaya ila nategemea afanye mazuri kwa ajili ya mtoto wetu,”alisema Malick.
Malick alifungua kinywa kufuatia madai kwamba alipokuwa akiishi na Rose alikuwa akimpa sheria kali na kumkataza kwenda ‘out’ ndiyo maana alikuwa hajiachii kama ilivyo sasa na hiyo ni moja ya sababu zilizosababisha uhusiano wao kuvunjika.
“Mimi siyo mkali wala sina sheria hizo ninazoambiwa ila nilikuwa nachukua muda mwingi sana kuzungumza na Rose na ninaamini amejifunza mengi sana mazuri ambayo akiyazingatia yatamsaidia maishani.
“Sababu za Rose kujiachia hivyo ni kutokana na maisha ambayo tulikuwa tunaishi hivyo anahitaji muda atatulia na atakuwa sawa na hapo ndipo atakapoanza kuyafanyia kazi yale mazuri aliyoyapata kutoka kwangu, sitegemei yeye kufanya mabaya ila nategemea afanye mazuri kwa ajili ya mtoto wetu,”alisema Malick.
No comments:
Post a Comment