
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Peaceland ya mkoani Mwanza wakishangilia
baada ya kupata taarifa ya shule yao kushika nafasi ya tatu kitaifa
katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba wa mwaka 2014 yaliyotangazwa
jana...
Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2014 yakionyesha kuwa zaidi ya nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani huo Septemba mwaka huu, wamefaulu.
Dar es Salaam. Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2014 yakionyesha kuwa zaidi ya nusu ya wanafunzi waliofanya mtihani huo Septemba mwaka huu, wamefaulu.
Matokeo hayo yaliyotangazwa jana na Katibu
Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde yanaonyesha kuwa wasichana
wamefanya vizuri zaidi ya wavulana, huku ufaulu kwa jumla ukiwa
umeongezeka kwa asilimia 6.38 ikilinganishwa na mwaka 2013.
Katika matokeo hayo Shule ya Twibhoki iliyopo
mkoani Mara iliibuka ya kwanza kitaifa kati ya shule 15,867 zilizofanya
mtihani huo ikifuatiwa na Mugini, Peacland na Alliance zote za mkoani
Mwanza.
Shule ya tano ni Kwema ya Shinyanga ikifuatiwa na
St Severine ya Kagera, Rocken Hill ya Shinyanga, Tusiime ya Dar es
Salaam, Imani ya Kilimanjaro na iliyoshika nafasi ya 10 ni Palikas ya
Shinyanga.
Wakuu wa shule vinara wazungumza
Mkuu wa Shule Twibhoki iliyopo Mugumu - Serengeti,
Alphonce Magori alisema siri ya mafanikio hayo ni kila mwalimu kutambua
nafasi yake.
Akizungumza ofisini kwake muda mfupi baada ya
kutangazwa kwa matokeo hayo alisema: “Kwanza ni mapenzi ya Mungu na
uongozi wa shule kutambua nafasi ya kila mtumishi na wajibu wake na
tunapata muda wa kujitathmini kama malengo yanafikiwa,” alisema.
Alisema wanafunzi nao hupata nafasi ya kutoa
tathmini ya kile wanachofundishwa na wanapewa mazoezi ya mara kwa mara
ambayo husaidia kujua uwezo wao na namna ya kuwasaidia.
Mwaka 2008 na 2010 ilikuwa ya pili kitaifa na tangu mwaka 2007 imekuwa ikiongoza kiwilaya na kimkoa.
Mkurugenzi wa Shule ya Alliance iliyoshika nafasi
ya nne, James Bwire alisema baada ya mwaka jana kushika nafasi ya 15
waliweka mikakati. Alisema siri ya mafanikio hayo ni ushirikiano wa
wazazi, walimu kujituma, mazingira mazuri ya shule na Ofisi ya Ukaguzi
wa Shule Wilaya ya Nyamagana.
Meneja wa Shule ya Peacland ya Ukerewe ambayo
mwaka jana ilikuwa ya 23, Halima Salum alisema alitarajia kupata
mafanikio hayo kutokana na ufahamu wa wanafunzi waliomaliza mwaka huu.
Mchanganuo
No comments:
Post a Comment