Askofu Kakobe
Naendelea kuwaletea mahojiano kati yangu na Askofu Kakobe kuhusiana na maisha yake ya wokovu.
Divai aliyoitengeneza Yesu ni karibu mapipa saba!...
Divai aliyoitengeneza Yesu ni karibu mapipa saba!...
Divai hii haikuwa kileo au pombe maana aliudhihirisha utukufu wake.
Ingekuwa amewapa watu kileo, ingekuwa aibu kwake badala ya utukufu.
Ilikuwa ni divai mpya au divai tamu yaani juisi ya zabibu, tofauti na
divai iliyochanganyika au kuchachuka ambayo ni pombe angalia Mithali
9:4-6; 23:29-30; Yoeli 3:17-18). Hatupaswi kunywa mvinyo au divai
iliyochanganyika ambayo ni kileo.
Mwandishi: Kuna baadhi ya watu huwa wanasema wamewahi kukutana au
kumuona Mungu, je, inawezekana watu kumuona Mungu hapa duniani?
Askofu Kakobe: Mtu hawezi kumuona Mungu ambaye ni roho kwa macho ya
kimwili, akaishi, kwa macho ya kimwili, mtu anaweza kumuona Mungu kwa
sehemu tu ya umbo na siyo uso angalia Hesabu 12:8; au Kutoka 33:17-23.
Hata hivyo, mtu anaweza kumuona Mungu anapokuwa katika roho, kwa macho
ya rohoni.
Mahali popote mtu alipomuona Mungu, alimuona katika hali hii, macho
ya mwili na mwili wote ukiwa hauna sehemu katika jambo hili angalia
Ufunuo 1:9-10; 2 au Wakorintho 12:1-4; au Matendo7:56. Katika roho, mtu
ndipo pia anaweza kusema na Mungu uso kwa uso kama rafiki yake kama
ilivyoandikwa katika Kutoka 33:11. Tunalojifunza hapa ni kwamba, Musa na
watu wengine waliomuona Mungu kwa macho ya rohoni, walifanya hivyo kwa
muda kidogo tu na wakarudia macho ya mwilini.
Mwandishi: Watu wengi sana wamezungumzia Jehanam, hebu tufafanulie, huko ni wapi na kukoje kwa mujibu wa ulivyosoma?
Askofu Kakobe: Mwanangu, huko kunatisha, nashindwa hata nikueleze vipi unielewe. Kuna moto wa milele, hatukuwekewa wanadamu bali shetani soma Mathayo 25:41. Kama utakwenda huko baada ya kusoma “note” hii, itakuwa ni kwa sababu ya kiburi chako tu na kushupaza shingo yako na kukataa kulitendea kazi Neno hili. Moto wa Jehanam siyo mahali pa mchezo kama walimu wa uongo wanavyofundisha.
Askofu Kakobe: Mwanangu, huko kunatisha, nashindwa hata nikueleze vipi unielewe. Kuna moto wa milele, hatukuwekewa wanadamu bali shetani soma Mathayo 25:41. Kama utakwenda huko baada ya kusoma “note” hii, itakuwa ni kwa sababu ya kiburi chako tu na kushupaza shingo yako na kukataa kulitendea kazi Neno hili. Moto wa Jehanam siyo mahali pa mchezo kama walimu wa uongo wanavyofundisha.
Mwandishi: Wapo watu wanaosema kuwa Jehanamu watu wakitupwa huko, wataungua kisha kuteketea kabisa, unasemaje kuhusu hilo?
Askofu Kakobe: Kwa ujumla, mafundisho yote haya yanatokana na
shetani, yanalenga kuwafanya watu waendelee kutenda dhambi, huku
wakipuuza ukweli juu ya Jehanam, kwa kuwaza kwamba watateseka dakika
chache na kupotea kabisa na ndiyo mwisho. Jehanum ya moto, au kuzimu, ni
shimo kubwa na refu sana lililojaa moto. Moto wa Jehanam huchochewa
mfululizo, ili usizimike; lakini huchochewa na pumzi ya Bwana, yaani
pumzi maalum ya Mungu mwenyewe soma Isaya14:15.
Mwandishi: Maandiko yanasemaje kuhusu Jehanamu?
Mwandishi: Maandiko yanasemaje kuhusu Jehanamu?
Askofu Kakobe: Maandiko yanasema ukali wa moto wa Jehanam, unatisha
angalia Waebrania 10:26-27. Moto wa Jehanam ni tofauti kabisa; Ni moto
wa rangi nyeusi, unaosababisha giza na kumfanya mtu aliye motoni, awaone
wenzake wachache tu wa karibu naye, hivyo hamna faraja ya kusema “tuko
wengi!” Moto huu mweusi, ndiyo maana unaitwa “giza la nje” angalia
Mathayo 8:11-12 . Walioko huko motoni, wakimuona yeyote mwingine kutoka
duniani, ambaye alikuwa na nafasi ya kusikia habari kama hizi na
akazipuuza, kisha akawafuata huko motoni, humwambia, “Je, wewe nawe
umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe umekuwa kama sisi!” (soma Isaya 14:
10).
Mwandishi: Kuna hili suala la Tanganyika kutaka kurejeshwa, limesemwa
katika Rasimu ya Katiba iliyotengenezwa na Tume ya Warioba, wewe
unasemaje kuhusu suala hilo? Askofu Kakobe: Inachekesha sana, huku kwetu
(Tanganyika) ni nchi gani? Kwa nini tukubali Zanzibar nchi na huku
kwetu ni nini?
Wanasema kuna mambo ya muungano na mambo yasiyo ya muungano, wanasema
kuna mambo yasiyo ya muungano yanashughulikiwa na Zanzibar na mambo ya
muungano yanashughulikiwa na nani na nchi gani? Haiko, imeyeyuka hewani
ikapotelea na Nyerere kwa sababu siyo mpango wa Mungu ndiyo maana miaka
nenda miaka rudi kumekuwa na vikundi vinavyoibuka hata ndani ya uongozi
wa serikali kutaka Tanganyika irudishwe.
Utaona tume moja baada ya nyingine, Tume ya Nyalali, Tume ya Kisanga,
tume chungu nzima siyo kitu kimeanza na Jaji (Joseph) Warioba,
ilianza tangu Nyerere mpaka ikaja G 55 wabunge vigogo wa CCM walitaka
Tanganyika enzi za Nyerere aliyekuwa anaogopwa kama simba lakini watu
walidai Tanganyika. Nyerere ilikuwa shughuli lakini bado akiwa bado
anaishi kukatokea watu 55 wakadai Tanganyika kwa sababu ni Mungu
anayetaka iwe.
Mwandishi: Wewe unadhani hili la kudai Tanganyika litakuwa mwisho wake Dodoma kwenye Bunge Maalum la Katiba?
Askofi Kakobe: Hapana. Kelele za Tanganyika zitaendelea na hakuna mtu
atakayezima. Kila anayepigania Tanganyika ana Mungu ndani yake, ni
suala la muda tu, Tanganyika lazima irudi huo ni urithi wa Mungu
aliyetuwekea mipaka. Anayeipigania Tanganyika nampongeza kwa sababu
Mungu yupo ndani yake.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment