Friday, 31 October 2014

KIPA STAND: TEGETE ALITAKA KUNIUA

Mshambuliaji wa Yanga, Jerry....
Tegete
KIPA wa Stand United, John Lwenda, amesema kuwa mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete alikuwa akihaha kutafuta bao kwa kupiga mashuti makali langoni mwake kiasi kwamba alihisi anataka kumtoa uhai.
Kauli hiyo imekuja baada ya Yanga kushinda mabao 3-0 dhidi ya Stand, kwenye Uwanja wa Kambarage, wikiendi iliyopita ambapo Tegete alifunga mabao mawili huku Geilson Santos ‘Jaja’ akifunga moja.
Kipa huyo ameliambia gazeti hili kuwa, Tegete ni straika anayejua jinsi ya kujipanga na kudai kuwa licha ya kuingia kipindi cha pili katika mechi hiyo, makeke yake yalikuwa hatari na alikuwa akipiga mashuti kila mara.
“Tegete sijui alitaka kuniua! Maana alikuwa akipiga mashuti makali kila alipopata. Si kwamba mabeki walishindwa kumkaba ipasavyo, hapana, ila jamaa anajua,” alisema kipa huyo.

No comments:

Post a Comment