KASHFA
iliyoibuliwa na Wakala wa Uchunguzi wa Mazingira ya Uingereza,
(Environmental Investigation Agency kwa kifupi EIA), dhidi ya serikali
kuhusu ziara ya Rais wa China, Xi Jinping hapa nchini kuwa msafara wake
uliondoka na shehena ya meno ya tembo ni nzito inayolitia doa taifa....
Kwa uzito wake, nafsi yangu kama mzalendo na muumini wa heshima kwa
viongozi wangu na taifa langu nilitaraji majibu ya serikali yangeendana
na ukubwa wa kashfa hiyo inayolidhalilisha taifa letu.
Kwangu mimi, naona siyo sawa kuituhumu ripoti ya EIA na kuiita ni ya kupikwa bila kuonesha kinagaubaga kupikwa huko ni kwa namna gani na kumetokana na nini?
Kwangu mimi, naona siyo sawa kuituhumu ripoti ya EIA na kuiita ni ya kupikwa bila kuonesha kinagaubaga kupikwa huko ni kwa namna gani na kumetokana na nini?
Kama hilo halitoshi, siyo sahihi pia kuishia kwenye kikomo cha uongo
wa taarifa bila kuvitaka vyombo husika vilivyoripoti habari hiyo vieleze
ukweli wa jambo hilo, kwa kuwa ni wazi sheria za vyombo vya habari
duniani zinakataza kutangaza taarifa ya uongo.
Nasema hivyo kwa sababu maudhui ya habari iliyotangazwa ni mapana
zaidi. Lingekuwa jambo la kawaida kama mkono wa taarifa hiyo ungekuwa
unawahusisha watu fulani kwa aina ya uraia wao lakini siyo taasisi nyeti
za nchi kama ikulu.
Ni jambo zito na la fedhaha kubwa kuutangazia ulimwengu kuwa msafara
wa rais wa China ambao kiprotokali ulipokelewa na kusindikizwa na rais
wa Tanzania na maofisa wa ngazi za juu wa usalama kuwa ulihusika na
uhujumu uchumi, halafu majibu ya serikali yakaishia kwenye kauli za
kusema habari hiyo ni ya uongo na wivu tu bila kuvuka mpaka huo.
Kama mzalendo, majibu hayo hayajaniondolea aibu kwa nchi yangu;
hayajamrudishia heshima rais wangu na yameshindwa kurejesha heshima ya
Watanzania kimataifa kwa sababu ni mepesi mno!
Ninaposema mepesi nina maanisha kwamba, majibu hayo yana maswali ndani yake; hayamalizi mjadala na hayamtaji mkweli ni nani kati ya EIA, vyombo vikubwa vya habari vya nje na serikali.
Ninaposema mepesi nina maanisha kwamba, majibu hayo yana maswali ndani yake; hayamalizi mjadala na hayamtaji mkweli ni nani kati ya EIA, vyombo vikubwa vya habari vya nje na serikali.
Kama tunaweza kuwa na taasisi, vyombo vya habari vinavyoweza
kuingilia uhuru wa nchi yetu kwa kiwango hicho na kuviacha bila
kuvichukulia hatua zinazoshtahili, kama taifa tunawezaje kujenga
heshima?
Katika sakata hili bado kuna mambo mawili ya kuamini kutokana na
mazingira yalivyo; Kwanza ni kuwepo kwa ukweli wa tuhuma za uhujumu
uchumi zinazolihusisha taifa kubwa kinara wa soko la meno ya tembo
duniani kwa kushirikiana na watawala wetu kujihusisha na biashara
haramu.
Pili ni kupikwa kwa skendo hiyo kwa malengo yasiyojulikana kama majibu ya serikali yalivyodai na hivyo kulifanya taifa lionekane sawa na simba wa chuma ambaye hata watoto wanaweza kumchezea watakavyo.
Pili ni kupikwa kwa skendo hiyo kwa malengo yasiyojulikana kama majibu ya serikali yalivyodai na hivyo kulifanya taifa lionekane sawa na simba wa chuma ambaye hata watoto wanaweza kumchezea watakavyo.
Kwa mtazamo; mambo yote mawili ni ya aibu! Ikiwa ni kweli viongozi
wetu wamefika mahali pa kushirikiana na wahujumu uchumi kufanya hata
biashara haramu ujue kaburi la maendeleo ya taifa limeshachimbwa na muda
mfupi ujao nchi itazikwa na aibu itakuwa juu ya viongozi wa awamu hii.
Aidha, kama jambo hili haliko hivyo na kwamba kuna wahuni wamepika
taarifa hizo kwa lengo la kufanikisha matakwa yao, bado pia ni jambo la
aibu kama serikali ya China na Tanzania zitakubali kufanyiwa uzushi
mkubwa kiasi cha kuihusisha hadi ndege ya rais kubeba mali za magendo,
huku maofisa wa usalama wakitajwa kuhusika moja kwa moja na biashara
haramu.
Kwa mtazamo huu, kama serikali inaziamini kauli zake juu ya kashfa
hii nzito kuwa habari ni za uongo njia pekee ya kuufuta uongo huo ni
moja; nayo ni ya kuujulisha ulimwengu kwa vielelezo kuwa taarifa hizo
siyo sahihi kwa kuweka ushahidi mezani.
Ikishindwa kufanya hivyo itajikuta imeangukia katika kipengele kimoja
wapo kati ya nilivyovitaja; cha kuhusika ambacho ubaya wake ni watawala
wa nchi kujihusisha na ufisadi au kutohusika ambako kutawaweka pia
viongozi wa nchi katika fungu la watu dhaifu wanaoweza kuzushiwa vitu
vibaya kama hivyo wakanyamaza.
Nashauri; hatua zaidi ya kauli za serikali zichukuliwe ili kuiondoa
kashfa hii. Kwanza utangazwe mgogoro na taasisi ya EIA juu ya taarifa
zake, kushinikiza iwasilishe kwenye vyombo vya kimataifa ushahidi wa
taarifa hiyo na ikishindwa kufanya hivyo hatua za kisheria zichukuliwe
sambamba na vyombo vya habari vilivyoripoti habari za uongo dhidi ya
serikali ya Tanzania, vinginevyo, hatuweza kujivika nguo kwa maneno bali
vitendo.
No comments:
Post a Comment