Monday, 10 November 2014

ESHA AJIAPIZA KIAPO CHA KIFO

Staa wa Bongo Movie,...
Esha Buheti.
STAA wa Bongo Movies, Esha Buheti amejiapiza kiapo cha kifo kwa kusema kuwa kama ipo siku atajaribu mchezo wa usagaji basi atakapomaliza tu litokee gari na kumkanyaga na kufa.
Akizungumza na mwandishi wetu, Esha alisema kuwa alishajiapiza kwa kutumia Msahafu ya kuwa kamwe hawezi kufanya tendo hilo akiamini kuwa liko kinyume kabisa na Mwenyezi Mungu. “Kwa kweli mimi nikifanya usagaji siku hiyo nikimaliza tu wakati natoka basi lije gari tena kubwa na kunigonga nife kabisa,” alisema Eshe.
Hivi karibuni vitendo vya kisagaji vimeshamiri kwa kasi huku mastaa wengi wa filamu wakitajwatajwa kujihusisha navyo.

No comments:

Post a Comment