Friday, 14 November 2014

BABA MSUVA AELEZA KISA CHA SIMBA, MWANAYE

Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva.
BABA wa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva ambaye ni Happygod Msuva ameeleza kushangazwa na taarifa kuwa Simba inataka kumsajili mtoto wake....
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Pope, alinukuliwa akisema kuwa, baada ya kumsainisha mkataba mpya kiungo wao, Jonas Mkude, sasa wanamhitaji Msuva.
Hans Pope alisema kuwa, dau la kuanzia kumsajili Msuva walilotenga ni shilingi laki tano, hivyo wanajipanga kutuma maombi Yanga. Akizungumza na Championi Ijumaa, Happygod alisema aliwahi kumpeleka mwanaye kwenye timu hiyo lakini walimwekea pozi.
“Unakumbuka kipindi kile Simon alikuwa akizomewa mara kwa mara na mashabiki wa Yanga? Basi nikaamua kwenda kuzungumza na aliyekuwa Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, walitoa majibu ya dharau kila nilipowapigia simu.
“Yanga imechangia kumlea Simon mpaka hapo alipo baada ya kuanzia katika Academy ya Azam FC, nilipoona hakuna maendeleo wakati akiwa chini ya Idd Cheche na Kali Ongala, nikampeleka Moro United ndipo Seif Magari akamchukua na kumpeleka Yanga.
“Hivyo kama Simba wanamtaka, wawafuate Yanga kwa kuwa bado ana mkataba, lakini ukweli ni kuwa ninawashangaa hao Simba wanamtaka Simon kwa kipi!” alisema Happygod.

No comments:

Post a Comment